Mon, 14 Mar 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Jeshi la Polisi mkoani Kilimanjaro limewataka maofisa wake waliopangiwa kazi katika ngazi ya kata kutekeleza majukumu yao kwa kufuata maadili ya jeshi hilo ikiwa ni pamoja na matumizi ya lugha nzuri kwa jamii, kuacha vitendo vya ulevi na kujiingiza kwenye mahusinao na wanafunzi.
Hayo yameelezwa na kaimu kamanda wa Polisi mkoa wa Kilimanjaro Kamishna wa Polisi Yahaya Mdogo wakati wa kikao na Wakaguzi wa jeshi la Polisi, kikao kilicholenga kuwakumbusha wajibu wao wa kuzuia na kupambana na uharifu.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live