Mahakama ya Wilaya ya Musoma mkoani Mara imemhukumu Nyangi Juma kwenda jela miaka saba na kulipa faini ya shilingi milioni tatu kwa muathiriwa baada ya kukutwa na hatia ya kufanya vitendo vya unyanysaji na kusababisha ulemavu wa kudumu kwa mtoto aliyekuwa akimlea.
Mahakama ya Wilaya ya Musoma mkoani Mara imemhukumu Nyangi Juma kwenda jela miaka saba na kulipa faini ya shilingi milioni tatu kwa muathiriwa baada ya kukutwa na hatia ya kufanya vitendo vya unyanysaji na kusababisha ulemavu wa kudumu kwa mtoto aliyekuwa akimlea. Akisoma hukumu hiyo Hakimu Mkazi Mwandamizi, Hadija Masala amesea tukio hilo limetokea Mei 16, 2023 katika Mtaa wa Iringo, Manispaa ya Musoma mkoani Mara ambapo Nyangi alikuwa akiishi na watoto wawili na mmoja kati yao alikuwa mtoto wake wa Kumzaa.