Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Jela miaka 30 kwa kubaka mwanafunzi

MIMBDFA.png Jela miaka 30 kwa kubaka mwanafunzi

Thu, 10 Sep 2020 Chanzo: dar24.com

Mkazi wa kijiji cha Isesa wilaya ya Misungwi Mkoani Mwanza Bujiku Mpeka amehukumiwa jela miaka 30 kwa kosa la kubaka, kutorosha na kuishi na mwanafunzi mwenye umri wa miaka 16,wakati wa likizo ya corona.

Hakimu wa mahakama ya wilaya ya Misungwi Esther Maliki amesema Peleka amewekwa hatiani baada ya upande wa mashtaka kupeleka mashahidi wanne akiwemo mwanafunzi mwenyewe anae soma kidato cha pili shule ya Sekondari Sumbugu.

“Tukiwa kwenye likizo ya corona Machi 22, Bujiku anipeleke kwao kijiji cha Isesa tukasalimie na tulipofika akanizuia kurudi nyumbani tukaishi nae hadi tulipokamatwa na polisi”. Amesema Mwanafunzi.

kwa upande wake mtuhumiwa aliiomba mahakama imsamehe kwani hatachukua tena mwanafunzi na kuishi nae.

Naye muendesha mashtaka Mkaguzi wa Msaidizi wa Polisi Juma Kipalo, ameiomba mahakama kuendelea kutoa adhabu kali ili ikukomesha tabia hii.

Chanzo: dar24.com