Sat, 11 Jun 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mahakama ya Wilaya ya Iringa imemuhukumu kifungo cha maisha na fidia ya Tsh. Milioni 10, Ramadhan Musa Chewa (34), Mkazi wa Pawaga, Iringa kwa kosa la kumuingilia kinyume na maumbile mtoto wa kike wa dada yake mwenye umri wa miaka 12.
Hakimu Mkazi Mkuu, Ally Said Mkasiwa amemesema mtuhumiwa alitenda kosa hilo Aprili 4, 2020 alipoenda kumsalimia dada yake, ambapo alikuwa akilala sebuleni.
Siku ya tatu baada ya kuwasili, dada yake alipotoka kwenda kuchota maji asubuhi, mtuhumiwa akaingia chumbani na kutenda kosa hilo.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live