Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Jamaa amuua mama mkwe wake kwa mapanga

SDDD MUUAJI Jamaa amuua mama mkwe wake kwa mapanga

Wed, 8 Feb 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Mwanamume huyo kwa jina Mthandazo Joseph Baskete alivamia nyumba alimokuwa akiishi mchumba wake - mwenye umri wa miaka 32 - waliyekuwa wamezozana, mama yake na mtoto wao mvulana wa miaka mitano.

Akithibitisha tukio hilo, msemaji wa polisi wa Limpopo Kanali Malesela Ledwaba amesema kuwa mshukiwa aliwashambulia wahasiriwa kwa panga kabla ya kutenya nyara mwanawe.

"Mshukiwa kisha akalazimisha mtoto wao wa miaka mitano kungia kwa gari la aliyekuwa mchumba wake na kuendesha kwenda naye," Ledwaba amesema.

Hata hivyo mshukiwa huyo aliliacha gari hilo kilomita chache kutoka eneo la tukio kabla ya kumpeleka mwanawe nyumbani kwa babake.

Wanawake hao wawili walikimbizwa katika kituo cha afya kilichokuwa karibu lakini mama mkwe wake akaaga dunia kutokana na majeraha.

Polisi wanasema kuwa msako umeanza ili kumtia mbarani mwanamume huyo ambaye atakabiliwa na mashtaka ya mauaji, jaribio la mauaji, utekaji nyara na wizi wa gari.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live