Tue, 9 Nov 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mmoja wa majaji waliokaa muda mrefu katika mahakama ya jinai ya Umoja wa Mataifa, Theodor Meron anatarajia kujiuzulu hivi karibuni.
Nia kujiuzulu ya jaji huyo mzaliwa wa Marekani iliwasilishwa kwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres ambapo amesema anatarajia kujiuzulu Kuanzia Novemba 17, 2021.
Iwapo ombi lake hilo litakubaliwa, atakuwa anaadhimisha miongo miwili tangu kuanza kwa muhula wake wa kwanza kama Jaji wa Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu wa Yugoslavia ya zamani (ICTY).
Chanzo: www.tanzaniaweb.live