Jaji Elinaza Luvanda wa Mahakama Kuu Divisheni ya Uhujumu Uchumi na Makosa ya Rushwa aliyekuwa anaisikiliza kesi ya Uhujumu Uchumi namba 16/2021 yenye mashtaka sita yakiwemo ya ugaidi, amejitoa kusikikiza kesi hiyo.
Hatua hii imekuja mara baada ya Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe kwa niaba ya wenzake kumuomba Jaji huyo ajitoe kusikiliza kesi yao ili kulinda heshima yake na ya Mahakama.
Mbowe na wenzake wanashitakiwa kwa makosa ya Ugaidi pamoja na Uhujumu uchumi, na hapo awali walifikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kabla ya Kesi hii kuhamishiwa katika Mahakama hii yenye Hadhi ya kusikiliza Makosa wanayoshitakiwa nao kwa mujibu wa taratibu za kimahakama.