MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu inatarajia kutoa hukumu kesho ya mshitakiwa Bogias Augustine na wenzake wawili wanaokabiliwa na mashitaka matatu ikiwemo kumwekea dawa za kumlevya Hunaina Salehe na kumuibia kifaa cha sauti pamoja na simu aina ya Iphone 11 pro max yenye thamani ya Sh 2,280,000 na fedha taslimu Sh 200,000.
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu inatarajia kutoa hukumu kesho ya mshitakiwa Bogias Augustine na wenzake wawili wanaokabiliwa na mashitaka matatu ikiwemo kumwekea dawa za kumlevya Hunaina Salehe na kumuibia kifaa cha sauti pamoja na simu aina ya Iphone 11 pro max yenye thamani ya Sh 2,280,000 na fedha taslimu Sh 200,000. Pia Bogius anakabiliwa na mashitaka ya unyang’anyi wa kutumia silaha ambapo alimtishia Hunaina kwa kisu ili abaki na mali hizo. Washitakiwa wengine ni Ally Kibuga na Abdallah Mmangi wanaodaiwa kushirikiana kupokea simu ya wizi aina ya Iphone 11 pro max yenye thamani ya Sh 2,280,000 kutoka kwa Bogias huku wakijua kuwa simu hiyo ni ya wizi.