Mon, 18 Oct 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kesi inayomkabili Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe na wenzake ya uhujumu uchumi yenye mashtaka ya ugaidi iliyokuwa imepangwa kutolewa uamuzi wa kesi ndogo tarehe 19, 2021 imepelekwa mbele hadi Oktoba 20,2021
Mahakama imefikia hatua hii ili kupisha sikukuu ya Maulid ambayo itafanyika Oktoba 19, 2021.
Inaelezwa kuwa tayari Mkuu wa Mahakama ya Division ya uhujumu uchumi ameshawapatia taarifa rasmi ya wito Mawakili, watuhumiwa pamoja na magereza juu ya mabadiliko hayo ya tarehe.
Kesi hii itaendelea tena tarehe tajwa majira ya saa tatu mbele ya Jaji Christopher Siyani.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live