Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Gunia tano za bangi zakamatwa Longido

Gunia Gunia tano za bangi zakamatwa Longido

Thu, 27 May 2021 Chanzo: ippmedia.com

Akizungumza na Nipashe meneja ambaye ni askari wa hifadhi hiyo, Peter Millanga, amesema majira ya saa tano usiku wa kuamkia leo, askari wamefanikiwa kukamata pikipiki ikiwa na gunia tano za bangi eneo la Engutukoit ukanda wa Ngereyan ambazo zilikuwa zikisafirishwa kwa njia za panya kuelekea Kenya.

"Mhusika hakuweza kukamatwa kwani alipozidiwa alitelekeza pikipiki na mzigo wake na kufanikiwa kukimbia," amesema Millanga.

Millanga amesema kwa mujibu wa askari walioshiriki kwenye doria hiyo, wamesema walipokea taarifa toka kwa msiri wao (informer) na kuamua kuifanyia kazi taarifa hiyo ndipo walipofanikiwa kukamata magunia.

Chanzo: ippmedia.com