Polisi mkoani humo imemtia mbaroni mtu mmoja mkulima na mkazi wa kijiji cha Kabulanzwili wilaya ya Kasulu mkoani Kigoma akituhumiwa kupatikana na madawa ya kulevya aina ya bangi yanayokadiriwa kuwa na uzito wa tani moja.
Kamanda mkoa Kigoma Ramadhani Kingai akizungumza na waandishi wa habari mjini Kigoma alimtaja mtu aliyekamatwa kuwa ni Lije Nicholous maarufu kama Madeberi (48) mkulima na mkazi wa kijiji cha Kabulanzwili wilayani Kasulu mkoani Kigoma.
Kamanda kingai alisema kuwa mtuhumiwa alikamatwa na polisi waliokuwa doria akiwa kwenye harakati za kusafirisha madawa hayo ya kulevya kwenda kuuza ambapo haijalezwa mara moja yalikuwa yakipelekwa wapi.