Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Ditopile, DMC wametembelea wafungwa Gereza la Kondoa na kutoa futari

Wafungwa Ed Ditopile, DMC wametembelea wafungwa Gereza la Kondoa na kutoa futari

Sun, 25 Apr 2021 Chanzo: ippmedia.com

Akizungumza baada ya kukabidhi mahitaji hayo, Mbunge huyo ameahidi kushirikiana na uongozi wa Gereza hilo katika kukamilisha ujenzi wa zahanati inayojengwa ambayo pia itakua msaada mkubwa kwa wananchi wa maeneo jirani.

Ditopile amesema pia amepokea changamoto kutoka kwa Mkuu wa Gereza hilo, Julius Nachunga, ambaye ameomba msaada wa mashine ya kupasulia mawe kwani wanao mradi wa kupasua mawe ambao kama wakipata mashine wataufanya kwa ufanisi zaidi na utawaingizia kipato kikubwa ambacho kitawasaidia kama Gereza katika kujiendesha.

” Mimi kama Mbunge wa Mkoa wa Dodoma na mwanachama wa DMC leo tumefika kuwasilimu wafungwa na mahabusu, pamoja na kuwafariji pia tumewaletea mahitaji mbalimbali ikiwemo futari kama tunavyofahamu huu ni mwezi Mtukufu wa Ramadhan, nguo za aina zote kama kanzu kwa ajili ya kuswalia, taulo za kike kwa ajili ya wafungwa wanawake, tunafanya hivi kwa upendo tukitambua hawa ni ndugu zetu na wanahitaji faraja" amesema Ditopile.

Kama gereza wana miradi yao ikiwemo wa kupasua mawe, lakini hawana vifaa kama Mashine ile ya kupasulia na badala yake wanatumia mikono, nimemuahidi pia Mkuu wa gereza kushirikiana nao tuweze kupata mashine hiyo ili waitumie pia katika kuwaingizia kipato kitakachowasaidia katika mahitaji yao mbalimbali.

Chanzo: ippmedia.com