Thu, 25 Jan 2018
Chanzo: bongo5.com
Msanii wa muziki Bongo, Chid Benz bado anashikiliwa na jeshi la polisi mkoani Dodoma kwa tuhuma za kukutwa na dawa za kulevya.
Jeshi la polisi mkoani humo limesema bado linaendelea kumshikilia msanii huyo na baada ya uchunguzi kukamilika atafikishwa mahakamani pamoja na washtakiwa wenzake.
Chid Benz alikamatwa December 30 mwaka jana, 2017 akiwa na mke wake na vijana wawili.
Chanzo: bongo5.com