Thu, 15 Sep 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam (RC), Amos Makalla amesema mkoa huo umeongeza askari 300 kwa ajili ya msako wa kuwakamata wahalifu maarufu 'panya road'.
Makalla ameyasema hayo leo Alhamisi Septemba 15, 2022 alipokuwa akizugumza na wananchi wa Kata ya Zingiziwa mara baada ya kutembelea ujenzi wa barabara ya Chanika-Homboza.
Amesema msako wa wahalifu huo umeanza tangu jana na kuwaambia wazazi ambao watapotelewa na vijana wao kuanzia leo Alhamisi wakawafuate vituo vya polisi au hospitali za wilaya.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live