Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

DPP awataka waliofanyiwa vitendo vya udhalilishaji kujitokeza

Mon, 26 Aug 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Mkurugenzi wa Mashtaka nchini Tanzania (DPP), Biswalo Mganga amewataka watu wote waliofanyiwa vitendo vya udhalilishaji ikiwemo kubakwa au kuingiliwa kinyume na maumbile kujitokeza na kutoa taarifa.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Jumatatu Agosti 26,2019 jijini Dar es Salaam, amesema hivi karibuni amejitokeza mtu (jina tunahifadhi) ambaye amekuwa akitumia majina tofautitofauti na kufanya vitendo vya udhalilishaji.

Amesema amekuwa akienda hoteli mbalimbali na kuwawekea wakina dada dawa kisha kuwabaka na kuwaingilia kinyume na maumbile kisha kuwaibia.

"Mara ya kwanza tulimfungulia mashtaka Mahakama ya Wilaya ya Kinondoni na kisha kuwekewa dhamana lakini baada ya kutoka aliendelea na vitendo vilevile," amesema Mganga

Amesema tayari wameshafuta kesi iliyokuwa Mahakama ya Kinondoni kisha kumfungulia kesi nyingine mbalimbali Agosti 21, katika Mahakama ya Kisutu ikiwemo ya uhujumu uchumi.

"Hakuna haki isiyokuwa na mipaka lazima kuangalia mtu kaathirika vipi wapo wengi hapa Dar es Salaam waliofanyiwa vitendo hivyo wakiwemo wake za watu," amesema

Pia Soma

" Wote waliofanyiwa vitendo hivi wajitokeze kesi hizi zitaendeshwa kwa siri majina yao na ya mashahidi hayatawekwa hadharani na Mahakama imekubali," amesema

Aidha Mganga amewataka watu kufuata sheria kwa kuwa amani na utulivu ni jukumu la kila mmoja.

Chanzo: mwananchi.co.tz