DJ wa zamani wa shirika la habari la BBC Alex Belfied ( 42) amehukumiwa kifungo cha miaka 5 na wiki 26 jela kwa makosa ya kuwanyanyasa watangazaji wanne wa mashirika mbalimbali ya habari ya nchini Uingereza.
Belfied alikutwa na makosa ya kugeuza mtandao kama silaha dhidi ya watu aliowalenga na kuendesha kampeni ya kuwanyanyasa na kuwasumbua bila kuchoka watangazaji hao, huku akiwasababishia mawazo na wasiwasi mkubwa.
Makosa hayo yalifanyika kati ya mwaka 2012 na 2021. Mmoja wa watangazaji hao alichanganyikiwa na kutamani hata kujiua kutokana na usumbufu huo ulioambatana na kurushiwa maneno ya chuki.