Fri, 2 Dec 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Zefrin Kimolo Lubuva ambaye aliwahi kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Manispaa ya Singida, ameshtakiwa kwa Matumizi Mabaya ya Ofisi na Ubadhirifu wa Tsh. Milioni 7.25
Fedha hizo alilipwa kama posho za kujikimu kwa miezi 6 kuanzia Desemba 2021 hadi Juni 2022 wakati uteuzi wake ulitenguliwa na Rais Februari 4, 2022
Mshtakiwa amekana makosa ambapo Mahakama imeagiza aliyekuwa Mweka Hazina na kuidhinisha malipo hayo aunganishwe kwenye Mashtaka. Kesi itatajwa tena Desemba 29, 2022.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live