Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

DC amtupa diwani wa Chadema mahabusu saa 48

9575 Dc+pic TZWeb

Wed, 20 Jun 2018 Chanzo: mwananchi.co.tz

Sumbawanga. Mkuu wa wilaya ya Sumbawanga, Halfan Haule ameagiza kukamatwa na kuwekwa ndani kwa saa 48 diwani wa Chadema.

Mkuu huyo wa wilaya alichukua uamuzi huo akimtuhumu diwani huyo kuandika barua yenye lengo la kuchonganisha waumini wa dini za Kikristo na Kiislamu hivyo kutishia kuhatarisha amani na utulivu uliopo.

Alitoa agizo hilo leo Juni 19, mchana katika kikao cha Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga, kilichofanyika kwenye ukumbi wa halmashauri hiyo mjini hapa.

Kwa mujibu wa Mkuu huyo wa wilaya, diwani huyo aitwaye Felician Mavazi  wa kata ya Kizwite anadaiwa kupeleka barua katika moja ya kanisa Katoliki wilayani humo, iliyowachonganisha waumini wa kiislamu na kikristo.

 

Chanzo: mwananchi.co.tz