Mon, 28 Jun 2021
Chanzo: globalpublishers.co.tz
Breaking: Mdude wa CHADEMA Aachiwa Huru June 28, 2021 by Global Publishers
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Mbeya,leo Juni 28, imemwachia huru kada wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Mdude Nyangali aliyekuwa akikabiliwa na kesi ya kusafirisha madawa ya kulevya aina ya Heroin gramu 23.4.
Hakimu mfawidhi wa mahakama hiyo, Zawadi Laizer amesema upekuzi uliofanyika nyumbani kwa mshtakiwa ulikuwa ni batili na haukufuata sheria na kanuni za upekuzi.
Chanzo: globalpublishers.co.tz