Kenya. Lydia Wangechi (80), ameieleza mahakama nchini Kenya jinsi mwanaye, William Gacheru alivyokuwa akimcharaza viboko bila huruma.
Ametoa kauli hiyo leo Jumanne Julai 16, 2019 wakati akitoa ushahidi wake katika Mahakama ya Karatina iliyopo Kaunti ya Nyeri, Kenya.
Wangechi amefungua kesi katika mahakama hiyo akidai mwanawe wa kumzaa amekuwa akimpiga na kumjeruhi.
Kwa mujibu wa ushahidi huo, Wangechi amedai Gacheru alikuwa akimtukana na kumpiga bila huruma tangu mumewe alipofariki dunia.
Mbele ya Hakimu Mkuu wa Karatina, Alice Mwangi, bibi huyo amedai Februai 6, 20q8 mtoto huyo alimpiga kichwani na kupata jeraha kubwa na kupelekwa Hospitali ya Karatina level 4 kwa ajili ya matibabu.
Huku akitoa ushahidi akiwa analia na kusababisha waliokuwepo mahakamani hapo wengi kuangua vilio, ameieleza mahakama kitendo hicho kimemuuma kwani hata mumewe ambaye waliishi katika ndoa kwa miaka mingi hakuwahi kumpiga.
Pia Soma
- Bongo movie, Swahilflix kumleta Will Smith Tanzania
- Rais Magufuli asisitiza bei elekezi zao la pamba ni Sh1,200
- NEC kuanza uboreshaji wa Daftari, Kihamia atoa mwongozo
- TCU yavifungulia vyuo vilivyofungiwa kudahili