Katika hali ya kusikitisha Mwanaume mmoja aliyefahamika kwa jina la Godbless Sawa Mkazi wa Kibamba Jijini Dar es salaam anadaiwa kumuuwa mke wake Ester Gadau kwa Kumpiga na jembe kichwani kisha naye kutokomea kusikojulikana.
Katika hali ya kusikitisha Mwanaume mmoja aliyefahamika kwa jina la Godbless Sawa Mkazi wa Kibamba Jijini Dar es salaam anadaiwa kumuuwa mke wake Ester Gadau kwa Kumpiga na jembe kichwani kisha naye kutokomea kusikojulikana. Ibada ya kumuaga Marehemu imefanyika Nyumbani kwao Mwananyamala ambapo baba wa marehemu aliyefahamika kwa jina la Benito Gadau amesimulia kwa uchungu namna alivyopewa taarifa juu ya tukio hilo huku akieleza kuwa wanandoa hao walikuwa na migogoro ya mara kwa mara hadi kufikia hatua ya kupelekana mahakamani na mahakama kuamua matatizo yao yamalizwe kifamilia.