Wed, 20 Jul 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mahakama ya Wilaya ya Arusha imemhukumu kifungo cha maisha jela Fadhil Sumayani (30 ) ambaye alikuwa mlinzi kwenye nyumba ambayo haijamaliziwa kujengwa kwa Kosa la kulawiti na kumbaka mtoto mwenye umri wa miaka tisa.
Tukio hilo ambalo linatajwa kufanyika Septemba 19, 2021 wakati Mtoto huyo alipotumwa na mama yake kwenda dukani kununua mahitaji ya nyumbani.
Akitoa hukumu hiyo ya Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama ya Wilaya ya Arusha Gwantwa Mwankuga amesema amemtia hatiani kwani ushahidi umethibitisha tukio hilo pasipo kuacha shaka yeyote.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live