Sat, 3 Dec 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Jeshi la Polisi mkoani Mbeya, linawashikilia Askari watano wa Jeshi hilo kwa tuhuma za kujihusisha na usafirishaji wa wahamiaji haramu ambao ni raia wa Ethiopia kuwapeleka nchini Malawi kupitia mpaka wa Kasumulu uliopo wilayani Kyela.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Kamishna Msaidizi wa Polisi, Benjamin Kuzaga, amethibitisha kukamatwa kwa Askari hao.
Aidha, Kuzaga ametoa wito kwa Askari kuacha kujihusisha na vitendo vya usafirishaji wa wahamiaji haramu.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live