Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Askari aliyembaka mtoto wa askari mwenzake afukuzwa kazi

97402 Pic+askari Askari aliyembaka mtoto wa askari mwenzake afukuzwa kazi

Fri, 28 Feb 2020 Chanzo: mwananchi.co.tz

Moshi. Askari wa kikosi cha usalama barabarani, Willium Mwakatage anayedaiwa kumbaka mwanafunzi wa darasa la saba, ambaye ni mtoto wa askari mwenzake amefukuzwa kazi.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Salum Hamduni amesema taratibu za kijeshi zimekamilika ikiwa ni pamoja na kumfukuza kazi.

Kamanda Hamduni amesema baada ya taratibu hizo kukamilika wanatarajia kumpandisha mahakamani leo Ijumaa Februari 28, 2020.

Mwakatage alikamatwa na polisi wa mkoa hapa Februari 15, 2020 ikiwa ni baada ya kupita zaidi ya siku 40

bila kuonekana kituo chake cha kazi, baada ya kusambaa kwa taarifa za tukio hilo.

Chanzo: mwananchi.co.tz