Dar es Salaam. Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam nchini Tanzania imewahukumu askari sita akiwemo mwanajeshi wa Jeshi la Wananchi la Tanzania (JWTZ) kulipa faini ya Sh500,000 kila mmoja baada ya kukiri shtaka la wizi wa mafuta ya ndege (Jet A-1/Ik).
Waliohukumiwa ni askari wa JWTZ, MT. 74164 SGT Ally Chibwana (47) na askari polisi, Koplo Shwahiba (38), Elidaima Paranjo (38), PC Simon (28), PC Dickson na PC Hamza.
Hukumu hiyo ilitolewa jana Ijumaa Oktoba 4, 2019 na Hakimu Mkazi, Vick Mwaikambo baada ya washtakiwa hao kukiri shtaka linalowakabili.
Mwaikambo alisema kwa kuwa washtakiwa hao ni kosa lao la kwanza hivyo mahakama hiyo imewapa adhabu ya kulipa faini ya Sh500, 000 kila mmoja na inawataka kulipa thamani ya zaidi ya Sh4 milioni ya mafuta ya ndege yaliyoibiwa na lita 109 zenye mafuta hayo yatarudishwa serikalini.
Awali, wakili wa Serikali Mwandamizi Renatus Mkude aliieleza mahakama hiyo kuna utaratibu wamekubaliana ili kumaliza shauri hilo.
Alidai kuwa awali washtakiwa hao walikuwa wanakabiliwa na makosa matatu hivyo walikubaliana kuliondoa shtaka la kwanza la kupanga genge la uhalifu na shtaka la tatu ni la utakatishaji wa fedha na shtaka la pili la wizi limebaki.
Pia Soma
- VIDEO: RAIS MAGUFULI: RUSHWA IMETENGANISHA NDOA ZA WATU
- Profesa Lipumba auzungumzia mgogoro uliokuwa CUF
- Magufuli atoa sababu ya kumtengua aliyetangaza Tanzania kuna Zika
- Rais Magufuli amtetea DED aliyechongewa na mbunge CCM