Morogoro. Askari wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), Kikosi cha Pangawe mkoani Morogoro, Leonald Liumba (52) ameuawa na mwili wake kukutwa umetupwa kwenye mashamba ya Mkonge ya Tungi.
Kutokana na mauaji hayo, Polisi mkoani hapa wanawashikilia watu watatu kwa tuhuma za mauaji hayo.
Kamanda wa polisi mkoani hapa, Wilbroad Mutafungwa leo Jumatano Juni 19, 2019 aliwaambi waandishi wa habari kuwa tukio lilitokea Mei 30, 2019 saa nne asubuhi eneo la Tungi katika mashamba ya mkonge Manispaa ya Morogoro ulikokutwa mwili huo ukiwa umetupwa.
Kamanda huyo amesema askari alitoweka nyumbani kwake tangu Mei, 25 mwaka huu.
Amesema mwili wake umekutwa umefungwa kamba mikononi na miguuni huku ukiwa na majeraha eneo la kisogoni na umeanza kuharibika.
Amewataja watuhumiwa ni Charles Luhunga maarufu Ubaya (36) na mwendesha bodaboda mkazi wa Msamvu Morogoro, Juma Said (25) maarufu Sokomoko mfanyabiashara katika Soko la Kikundi na Yusuph Makusi (24), mwendesha bodaboda eneo la Msamvu Morogoro na Dar es Salaam.
Pia Soma
- VIDEO: Shughuli Dar es Salaam zinaendelea kama kawaida
- Waziri Kigwangalla atoa siku saba kwa Tanapa, Tawiri
- VIDEO: Rugemalira awaweka benchi mawakili, asimama kujitetea mwenyewe
- Rais China aanza ziara Korea Kaskazini