Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Ashikiliwa kwa kujiandikisha mara mbili katika daftari la wapigakura Morogoro

80275 Pic+mvua

Wed, 16 Oct 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Morogoro. Ngeze Mwagilo (29) mkazi wa Kasanga Manispaa ya Morogoro anashikiliwa na polisi kwa tuhuma za kujiandikisha mara mbili katika daftari la wapigakura kwenye vituo viwili tofauti ndani ya manispaa ya Morogoro.

Kamanda wa polisi mkoani Morogoro, Wilibroad Mutafungwa amewaambia waandishi wa habari leo Jumanne Oktoba 15, 2019 ofisini kwake.

Amesema mtu huyo alikamatwa baada ya jeshi hilo kupata taarifa na kumfuatilia mtuhumiwa huyo wakati wa shughuli ya uandikishaji ikiendelea.

Mutafungwa amewatahadharisha wananchi mkoani humo wenye lengo la kutaka kuvuruga shughuli hiyo iliyoanza Oktoba 8 hadi 17, 2019 watachukuliwa hatua za kisheria kuwa polisi itahakikisha inawakamata huku akiwataka kuacha kufanya uhalifu huo.

Amesema mtuhumiwa huyo anadaiwa kujiandikisha katika kituo cha Kasanga kata ya Mindu na baadaye kwenda kujiandikisha katika kituo cha kiwanja cha Ndege kata ya Kiwanja cha Ndege Manispaa ya Morogoro.

Amesema mtuhumiwa huyo anaendelea kuhojiwa na atafikishwa mahakamani mara baada ya uchunguzi kukamilika ili sheria ichukue mkondo wake.

Pia Soma

Advertisement
Hata hivyo, kamanda huyo amesema shughuli hiyo ya uandikishaji katika daftari la mpiga kura linaendelea kwa amani na utulivu kwani hakuna matukio yoyote yalioripotiwa ya uvunjifu wa amani mkoani Morogoro huku jeshi lake likiendelea na ulinzi katika maeneo mbalimbali.

Chanzo: mwananchi.co.tz