Tue, 16 Jul 2019
Chanzo: mwananchi.co.tz
Dar es Salaam. Kampuni ya Mohammed Enterprises inamsaka mmoja wa wafanyakazi wake kwa tuhuma za kuiba injini 172 za pikipiki za kampuni hiyo.
Hayo yameelezwa leo Jumanne Julai 16, 2019 katika tangazo kwa umma lililotolewa na kampuni hiyo.
Tangazo hilo limemtaja mtuhumiwa huyo na kubainisha kuwa amefanya wizi huo Juni 15, 2019.
“Tukio hili limeripotiwa katika kituo cha polisi cha Chang’ombe na kupewa kumbukumbu namba CAG/IR/7557/2019,” linaeleza huku likitaja namba za injini hizo.
Pia Soma
- Bongo movie, Swahilflix kumleta Will Smith Tanzania
- Rais Magufuli asisitiza bei elekezi zao la pamba ni Sh1,200
- NEC kuanza uboreshaji wa Daftari, Kihamia atoa mwongozo
- TCU yavifungulia vyuo vilivyofungiwa kudahili
Chanzo: mwananchi.co.tz