Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Apigwa risasi, afariki kwa kukaidi amri ya JWTZ

16817 Pic+jwtz TanzaniaWeb

Tue, 11 Sep 2018 Chanzo: mwananchi.co.tz

Bagamoyo. Mkazi wa Bagamoyo ambaye jina halikutajwa amefariki baada ya kupigwa risasi akidaiwa kukaidi amri ya wanajeshi wakati akiingia kambi ya Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ)  Bagamoyo, mkoani Pwani.

Tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia leo Septemba 11, 2018 kwenye kambi ya JWTZ Mapinga Comprehensive Training Centre (CTC) kata ya Mapinga wilayani humo.

Kamanda wa polisi mkoani Pwani, Wankyo Nyigesa amekiri kutokea kwa tukio hilo na kwamba mtu huyu alipigwa risasi baada ya kuingia ndani ya kambi hiyo kwa kuruka ukuta usiku huo.

“Wakati anaruka alionekana na walinzi wa JWTZ waliokuwa zamu muda huo na walimuamuru asimame lakini alikaidi na kuanza kukimbia,” amesema  Nyigesa na kuongeza:

"Askari waliendelea kumsisitiza asimame lakini hakutii hivyo walilazimika kumsisitiza tena kwa kupiga risasi moja hewani, lakini hakuitii aliendelea kukimbilia walipo askari hivyo mmoja wa walinzi alimfyatulia risasi iliyompata kiunoni na kuanguka chini, "

Ameongeza kuwa baada ya kudondoka walimpekua lakini hakukutwa na silaha hivyo jitihada za kumpeleka hospitalini zilifanyika lakini alifariki njiani kutokana na kuvuja damu nyingi.

Kamanda Nyigesa aliwataka raia kutii amri na kufuata sheria wanapoingia kwenye kambi za jeshi.

Chanzo: mwananchi.co.tz