Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Kahama (KUWASA) imemtoza fidia ya shilingi milioni 1.2 mteja aliyeamua kujiunganishia huduma ya maji kwa kuchepusha (bypass) katika makazi yake.
Mteja huyo kwa jina Hamis Omari amekutwa kajiunganishia maji ambayo hayapiti katika Dira na kuyaelekeza katika maliwato na kuyatumia kwa kazi mbalimbali za nyumbani.
Ni kosa kuharibu miundombinu ya maji/kujiunganishia kwa mujibu wa Sheria Na. 5 ya mwaka 2019, Sheria ya Huduma ya maji na Usafi wa Mazingira
Bwana Hamisi Omari ni mkazi wa Mtaa wa Mwime Kata ya Mwendakulima
Katika wiki nne za mwezi Juni, 2023 Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Kahama ( KUWASA ) imekamata wananchi wawili kwa uharibifu wa miundombinu ya usambazaji majisafi.