Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Anayedaiwa kumuua mwanafunzi wa chuo akamatwa

63420 Pic+mwanafunzi

Wed, 19 Jun 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa amesema jeshi hilo linamshikilia mtu mmoja akidaiwa kumuua kwa kumchoma kisu maeneo ya kifuani Anifa Mgaya (21), aliyekuwa akisoma Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Kampala (KIU) tawi la Tanzania.

Juni 16, 2019 saa 3 usiku Anifa anadaiwa kuchomwa kisu upande wa kulia wa kifua chake na mtu huyo jina limehifadhiwa wakati akitoka kujisomea katika chuo hicho kilichopo GongolaMboto kisha kuporwa pochi iliyokuwa na simu na fedha Sh8,000.

"Baada ya kumhoji mshtakiwa amekiri kuhusika na tukio hilo, huku akieleza namna ambavyo mwanafunzi huyo wa mwaka pili (ngazi ya Stashahada ya Maabara) alivyokuwa amevaa siku hiyo," amesema Kamanda Mambosasa.

Mwili wa Anifa aliagwa jana Jumanne nyumbani kwao Salasala jijini Dar es Salaam kisha kusafirishwa kwenda Makambako mkoani Iringa kwa mazishi yanayotarajiwa kufanyika kesho Alhamisi.

Katika hatua nyingine, Kamanda Mambosasa amesema polisi linawashirikia watu 31 wanaodaiwa kujihusisha na vitendo vya kihalifu kwenye maeneo yanayopakana na vyuo vikuu katika jiji hilo na uchunguzi zaidi unaendelea.

Chanzo: mwananchi.co.tz