Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Aliyekutwa na almasi uwanja wa ndege apandishwa kizimbani

67063 ALMAS+PIC

Wed, 17 Jul 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Hany Ahmed (27), raia wa Misri amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu akikabiliwa na shtaka la kutorosha madini ya almasi yenye thamani ya zaidi ya Sh12 milioni.

Ahmed amefikishwa mahakamani hapo leo Jumanne Julai 16, 2019 na kusomewa shtaka  na wakili wa Serikali mwandamizi, Wankyo Simon.

Simon amedai mshtakiwa anakabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi.

Mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu wa mahakama hiyo, Thomas Simba, Simon amesema mshtakiwa anadaiwa kutenda kosa hilo Julai 10,  2019 Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), jijini Dar es Salaam.

Siku ya tukio, Ahmed alikutwa akisafirisha madini  hayo yenye uzito wa carats 11:12 ambayo yana thamani ya dola za Marekani 5,238 sawa na Sh12, milioni bila ya kuwa na kibali kutoka mamlaka husika.

Baada ya kusomewa shtaka hilo, raia huyo wa Misri hakutakiwa kujibu chochote kwa sababu mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza kesi za uhujumu uchumi.

Pia Soma

Wakili Simon amedai upelelezi wa kesi hiyo haujakamilika kuomba tarehe nyingine kwa ajili ya kutajwa.

Kesi hiyo imeahirishwa hadi Julai 30, 2019 itakapotajwa tena na mshtakiwa kurejeshwa rumande.

Chanzo: mwananchi.co.tz