Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Aliyehukumiwa miaka 20 kwa kubaka, akabiliwa na kesi mbili za kubaka

Fri, 21 Jun 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam.  Mshtakiwa James Stephano (24) anayetumikia kifungo cha miaka 20 jela kwa kubaka,  Julai 3, 2019 ataanza kujitetea katika Mahakama ya Wilaya ya Ilala Dar es Salaam katika kesi nyingine ya kubaka watoto wawili wa kike wenye umri wa miaka sita na tisa.

Stephano ambaye alikwisha hukumiwa  kifungo cha miaka 20 jela na Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo, Samwel Obasi katika kesi nyingine ya kubaka, siku hiyo ya Julai 3, 2019 ataanza kujitetea  katika  kesi ya  jinai namba 109 ya mwaka 2018  ambayo inasikilizwa mbele ya Hakimu Mkazi, Flora Mujaya na Wakili wa Serikali, Aziza Muhina.

Mshtakiwa huyo alipaswa kuanza kujitetea leo Alhamisi Juni 20, 2019 lakini ilishindikana baada ya Wakili wa Serikali Grace Lwila kueleza Mahakama hawajajiandaa hivyo ikasogezwa hadi Julai 3, 2019.

Katika kesi hiyo, Stephano anadaiwa kubaka watoto wawili wa kike kosa ambalo anadaiwa kulitenda kati ya  Julai na Agosti mwaka 2017 huko Gongolamboto jijini Dar es Salaam.

Ilidaiwa mahakamani hapo kosa hilo ni kinyume na kifungu cha 130(1)(2)(e) na 131 (1) cha sheria ya kanuni ya adhabu sura ya 16 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2002.

Hatua hiyo ilifikiwa mahakamani hapo baada ya shahidi wa upande wa mashtaka  ambaye ni askari kutoka  kituo cha Polisi cha Stakishali, kitengo cha Dawati la jinsia na watoto, WP 5034 D/Koplo Zainabu kutoa ushahidi wake na lipomaliza  upande wa mashtaka ukafunga kesi yao.

Pia Soma

Baada ya upande wa mashtaka kufunga ushahidi wao, Hakimu Mujaya alipitia ushahidi uliotolewa na mashahidi wa upande wa mashtaka na kutoa uamuzi kuwa mshtakiwa huyo ana kesi ya kujibu hivyo anatakiwa kujitetea.

Hata hivyo, baada ya Hakimu Mujaya kutoa uamuzi huo alimuuliza mshtakiwa huyo kama atakuwa na  mashahidi wangapi watakaotoa ushahidi upande wake naye alijibu atakuwa na shahidi mmoja aliyemtaja kwa jina la Ester.

Chanzo: mwananchi.co.tz