Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Aliyefungwa jela maisha aongezewa miaka 35 kwa kumuua mfungwa mwenzake

Operanews1670067661675 Aliyefungwa jela maisha aongezewa miaka 35 kwa kumuua mfungwa mwenzake

Sat, 3 Dec 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Peter Hiuhu Gachau, mfungwa aliyehukumiwa kifungo cha maisha jela katika gereza la King’ong’o GK huko Nyeri, ameongezewa tena kifungo cha miaka 35 jela.

Gachau, almaarufu ‘Undertaker’, alipatikana na hatia na Jaji wa Mahakama Kuu Florence Muchemi ya mauaji ya mfungwa mwenzake, Shem Mugendi, mnamo Agosti 17, 2015 jioni.

Mahakama iliarifiwa kwamba Gachau alimgonga Mugendi mara kadhaa kwa nyundo aliyokuwa ameingia kisiri nayo kisiri kutoka kwa karakana, huku uchunguzi wa maiti ukionesha majeraha mabaya ya kichwa aliyopata Mugendi.

Katika hukumu yake, Jaji Muchemi alisema kwamba alizingatia kwamba Gachau lazima alimsababishia Mugendi, ambaye alinyongwa akiwa amelala, maumivu mengi.

"Kitendo cha mshtakiwa lazima kilisababisha hasara na maumivu makubwa kwa mwathiriwa, ambaye pia alinyongwa na kufungwa pingu alipokuwa amelala," alisema Muchemi.

Usiku ambao Gachau alimuua Mugendi, walinzi walisema walisikia makabiliano makali ambapo alikiri kutekeleza mauaji hayo ya kutisha.

“Mshtakiwa alikimbia walipokuwa polisi na kusema ‘nimemmaliza’ kabla hajafungwa pingu na kisa hicho kuripoti kwa afisa wa magereza,” alisema hakimu huyo.

Gachau alikuwa akitumikia kifungo cha maisha jela baada ya kupatikana na hatia ya wizi wa kimabavu uliosababisha kifo cha mwalimu katika mahakama ya Nyeri mnamo Julai 8, 1999.

Waendesha mashtaka walikuwa wamekata rufaa kwa mahakama kumpa kifungo cha maisha jela wakisema kwamba bado alikuwa akionyesha tabia ya ukatili.

Hata hivyo, Jaji Muchemi alitofautiana na upande wa mashtaka akisema Gachau ameonyesha kuwa anajuta.

Muchemi alisema Gachau amekuwa akifanya vikao vya ushauri na wafungwa wenzake katika Gereza la King’ong’o GK.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live