Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Aliyedaiwa kujifanya ofisa Usalama wa Taifa akiri makosa

Mon, 7 Oct 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Upande wa mashtaka katika kesi ya uhujumu uchumi inayomkabili Thomas Magoli umedai kuwa mtuhumiwa huyo ameandika barua ya kukiri makosa na kuomba msamaha kwa mkurugenzi wa mashtaka nchini Tanzania (DPP), Biswalo Mganga.

Magoli anakabiliwa na makosa matatu likiwemo la kujifanya ofisa Usalama wa Taifa ili kumsaidia Rais wa zamani wa Shirikisho la Mapira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi katika kesi inayomkabili katika mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.

Wakili wa Serikali mwandamizi, Wankyo Simon amedai mbele ya Hakimu Mfawidhi, Kelvin Mhina kuwa mshtakiwa huyo alishaandika barua ya kukiri makosa kwa DPP lakini kuna baadhi ya vitu havijakamilika.

"Naiomba mahakama ipange tarehe nyingine kwa kuwa bado Kuna vitu havijakamilika," amedai Simon.

Kesi hiyo imeahirishwa hadi Oktoba 21, 2019.

Katika kesi ya msingi inadaiwa  katika kosa la kwanza kati ya Desemba 1, 2017 na Agosti 2019 mahabusu ya Keko jijini Dar es Salaam, mshtakiwa alijifanya mtumishi wa umma aliyeajiriwa kitengo cha Usalama wa Taifa.

Pia Soma

Advertisement
Shtaka la pili amedai kati ya Agosti 17,  hadi 29, 2019 katika maeneo tofauti jijini Dar es Salaam, mshtakiwa huyo alijipatia Sh280,500 kutoka kwa Lucy Ngongoseki akijifanya ofisa usalama anayetaka kumsaidia Malinzi anayekabiliwa na kesi namba 213/2017 ya uhujumu uchumi.

Katika kosa la tatu la utakatishaji fedha anadaiwa kutakatisha kiasi cha Sh280,000 kwa kuzitumia fedha hizo huku akijua fedha hizo ni zao la kosa tangulizi la kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu.

Chanzo: mwananchi.co.tz