Arusha. Kikosi cha kupambana na ujangili(KDU) Wilaya ya Kiteto kwa kushirikiana na askari wa hifadhi ya jamii ya wanyamapori (WMA) ya Makame iliyopo Kiteto wamemkamata mtuhumiwa wa ujangili, Masudi Mussa (33) akiwa na nyama ya pofu wanne.
Akizungumza na Mwananchi leo Jumatano Machi 11, 2020 ofisa wanyamapori wilaya ya Kiteto, Doris Gama amesema mtuhumiwa huyo alikuwa akisakwa kwa muda mrefu kutokana na kuhusika na matukio kadhaa ya ujangili.
Gama amesema alikamatwa na askari wa vikosi hivyo walioshirikiana na askari wa kupambana na ujangili wa taasisi ya Honeyguide.
“Kikosi cha doria wamemkamata na gobore moja, pikipiki mbili, risasi sita na visu vinne,” amesema.