Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Akamatwa Akisafirisha Bangi

Bangi Akamatwa Akisafirisha Bangi

Thu, 30 Dec 2021 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

POLISI katika kaunti ya Busia huko nchini Kenya wamemkamata mwanaume mmoja mwenye umri wa miaka 40 akisafirisha misokoto ya bangi aliyoificha kwenye begi na mingine kujizungushia mwilini.

Mwanamume huyo ambaye ametambuliwa kwa jina la Albert Wabwire amekamatwa asubuhi ya Alhamisi Desemba 30,katika eneo la Sio, akitembea kutoka Busia hadi Matayos nchini Kenya.

Polisi wanasema walipofanya upekuzi walimkuta akiwa na bangi kwenye begi alilokuwa amebeba huku kiasi kingine cha mzigo huo akiwa amefungwa kwa magunia kuuzunguka mwili wake.

Mtuhumiwa huyo kwa sasa anashikiliwa katika kituo cha polisi cha Busia akisubiri kufikishwa mahakamani siku ya Ijumaa Desemba 31, 2021.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live