Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Afungwa Jela miaka 30 kwa kupatikana na miche ya bangi

Bhangi Mtuhumiwa alihukumiwa Machi 15, Mwaka huu

Fri, 18 Mar 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya limefanikiwa kumkamata mtuhumiwa ANOSISYE AMOS MWAKITEGA [60] Mkazi wa Kyimo halmashauri ya Rungwe Mkoa wa Mbeya kwa kosa la kupatikana na miche ya bhangi 192 kinyume na kifungu cha sheria namba 11 (1) (a) cha sheria ya kudhibiti na kupambana na dawa za kulevya 2019.

Mtuhumiwa alikamatwa Machi 10, 2022 huko Kyimo halmashauri ya Wilaya ya Rungwe na kufikishwa mahakama ya Wilaya ya Rungwe ambapo alisomewa mashitaka matatu, 1. Kulima miche ya bhangi 192 kinyume na kifungu namba 11 (1) (a) cha sheria ya kudhibiti na kupambana na dawa za kelevya ya mwaka 2019, 2. Kupatikana na bhangi gramu 410 na 3. Kupatikana na bhangi gramu 12.3 kinyume na kifungu namba 17 (1) (a) na (b) ya mwaka 2019 iliyofanyiwa marejeo mwaka 2021.

Mnamo Machi 15, 2022 mtuhumiwa alipatikana na hatia kwa makosa yote matatu na kuhukumiwa kifungo jela miaka thelathini [30].

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi ULRICH MATEI anatoa rai kwa wananchi kuacha kujihusisha na biashara ya dawa za kulevya na badala yake watafute shughuli nyingine halali zitakazowapatia kipato halali. Aidha Kamanda MATEI anawataka wananchi kuacha mara moja matumizi ya dawa za kulevya kwani ni kinyume cha sheria n ani hatari kwa afya zao na watakapo kamatwa na kufikishwa mahakamani watafugwa.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live