Mon, 1 Aug 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Bad News! Mkazi wa Kibosho Kirima Juu, Wilaya ya Moshi mkoani Kilimanjaro anadaia kumuua mtoto wake mwenye umri wa miaka mitatu na miezi sita, kwa kumchapa na fimbo akimtuhumu kuchezea maji.
Mwanamke huyo mwenye umri wa miaka 27 anadaiwa kufanya mauaji hayo Julai 31, 2022, ambapo alimchapa na fimbo sehemu mbalimbali akimtuhumu kuchezea maji ya baridi.
Kamanda wa polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Simon Maigwa amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kubainisha kuwa mwanamke huyo tayari anashikiliwa na polisi.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live