Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Adaiwa kujiua kwa kujichinja kwa kisu

52560 Pic+kisu

Tue, 16 Apr 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Arusha. Mkazi wa mtaa wa Simanjiro, kata ya Sombetini jijini Arusha, Lazaro Kiolori (53) anadaiwa kujiua kwa kutumia kisu kidogo chanzo kikielezwa kuwa ni ugomvi wa kifamilia.

Kamanda wa polisi mkoa wa Arusha, Jonathan Shanna amesema leo Jumanne, Aprili 16, 2019 kuwa tukio hilo limeacha simanzi na mshtuko mkubwa kwa familia yake.

“Uchunguzi wa awali umeonyesha kuwa chanzo cha marehemu kujitoa uhai wake ni mgogoro uliokuwepo kati yake na wake zake wawili ambao sitawataja majina yao kwa sasa na mwili upo katika hospitali ya mkoa ya Mount Meru kwa uchunguzi zaidi,”amesema Shanna.

Amesema kuwa jeshi la polisi liliwahi kufika eneo la tukio na jitihada za kumwokoa hazikufanikiwa na kuwataka watu wenye msongo wa mawazo kuwatumia viongozi wa dini, wanafamilia na watalamu.



Chanzo: mwananchi.co.tz