Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

14 wapandishwa kortini, watuhumiwa kwa utakatishaji fedha

68116 Mahakama+pic

Wed, 24 Jul 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Watu 14  wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam nchini Tanzania wakikabiliwa na mashtaka manne ikiwemo la kusambaza taarifa zisizohitajika kwenye mitandao pamoja na utakatishaji fedha.

Washitakiwa waliofikishwa Mahakamani hapo leo Jumatano Julia 24, 2019 ni David Simon (32), Michael Joseph (22), Omary Rajabu (23), Ramadhani Issah(35), Adolph Martine (29), Martine Maiko (26), Ajuaye Gerald (23), .

Wengine ni;  Adam Christopher (27), Frank Magazi (29), Mathias Godfrey (22), Joseph Mabruck (26), John Mwambusa (50), Hamza Hassan (23), Amosi Mazwile (22).

Wakili wa Serikali ya Tanzania, Nancy Mushumbusi amedai mbele ya Hakimu Mwandamizi, Hamza Wanjahz kuwa katika tarehe tofauti kati ya mwaka 2017 na Mei 31, 2019 katika maeneo ya Sumbawanga mkoani Ruvuma na maeneo mengine ndani ya Tanzania washtakiwa hao walikula njama ya kutenda kosa la kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu.

Katika shtaka lingine kati  ya Januari 2017 na Mei 31, 2019 katika maeneo ya Sumbawanga mkoani Ruvuma na maeneo mengine ya Tanzania washtakiwa hao kwa pamoja kwa kujua na kwa makusudi walisambaza taarifa za uongo kwa njia ya ujumbe mfupi kwa kutumia kompyuta kwa lengo la kudanganya umma wakijua kufanya hivyo ni kosa.

Katika shtaka la tatu,  Wakili Mushumbusi amedai kati ya Januari 2017 na Mei  31, mwaka 2019 wakiwa Sumbawanga mkoani Ruvuma na maeneo mengine tofauti ndani ya Tanzania  washitakiwa  kwa pamoja walipanga kusambaza ujumbe usiohitajika kwenye mitandao  kwa njia ya kompyuta huku wakijua kufanya hivyo ni kosa kisheria.

Pia Soma

 Katika shtaka la nne, amedai kati ya Januari  2017 na Mei 31, 2019 wakiwa Sumbawanga na  katika maeneo tofauti ya Tanzania washtakiwa hao  walijihusisha katika miamala inayohusu fedha kiasi cha Sh11 milioni wakati wakijua fedha hizo si zao kosa la jinai la kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu.

Wakili Mushumbusi amedai upelelezi wa shauri hilo bado haujakamilika hivyo aliomba mahakama ipange tarehe nyingine kwa ajili ya kutajwa.

Hakimu Wanjah ameahirisha kesi hiyo hadi Agosti 7, mwaka 2019 kwa kutajwa na washitakiwa wamepelekwa rumande  kutokana na shtaka la utakatishaji fedha kutokuwa na dhamana.

Chanzo: mwananchi.co.tz