Mon, 2 Sep 2019
Chanzo: mwananchi.co.tz
Dar es Salaam. Polisi Kitengo cha Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya nchini Tanzania limewakamata watu 12 wakiwa na dawa za kulevya.
Dawa hizo ni heroin zenye uzito wa kilo 4.14, kilo 31.72 za Mirungi na gramu 55.26 za bangi.
Mkuu wa Kitengo cha Kuzuia Dawa za Kulevya cha Polisi Tanzania, Alhaj Kabaleke Salim akizungumza na waandishi wa habari leo Jumatatu Septemba 2, 2019 amesema kati ya watuhumiwa hao wanne ni raia wa Kenya, mmoja Mnigeria na tisa ni Watanzania.
Amesema watuhumiwa wote wanatarajiwa kufikishwa mahakamani ili kujibu tuhuma zinazowakabili.
Chanzo: mwananchi.co.tz