Timu ya Taifa ya Kriketi ya Australia imefanikiwa kuchukua ubingwa wa Dunia wa mashindano ya kombe la dunia la kriketi T20 baada ya kuifunga New Zealand.
Ubingwa huo umepunguza presha kwa kocha mkuu wa timu hiyo kutokana na kuwa na msimu mbaya na kupelekea baadhi ya wachezaji kuhoji staili ya ufundishaji wa kocha huyo.
Katika fainali hiyo iliyopigwa Falme za kiarabu, Dubai ilishuhudia Mitchell Marsh akiwatanguliza Australia kwa tofauti ya wickets nane dhidi ya New Zealand.
Hili linakuwa ni kombe la Dunia la kriketi la kwanza katika historia ya Australia, wakiwa wametwaa ubingwa huo kutoka kwa West Indies ambaye ndiye aliekuwa bingwa mtetezi.