Kampuni mbili kubwa za mtandao ambazo huko nyuma zilikuwa na ushindani mkubwa kwenye mitandao, Zoom na Kupatana zimeungana na kuwa chini ya kampuni moja ya Afrieuro Digital Ventures ambayo ndiyo imepata haki zote za kumiliki tovuti hizo zote mbili na kuongeza wigo mpana nchini Tanzania.
Kampuni mbili kubwa za mtandao ambazo huko nyuma zilikuwa na ushindani mkubwa kwenye mitandao, Zoom na Kupatana zimeungana na kuwa chini ya kampuni moja ya Afrieuro Digital Ventures ambayo ndiyo imepata haki zote za kumiliki tovuti hizo zote mbili na kuongeza wigo mpana nchini Tanzania. Kampuni hiyo imesema kuwa hii ni fursa nzuri zaidi kwa watumiaji wa mitandao kuweza kujipatia bidhaa mbalimbali kupitia tovuti hiyo.