Foleni za Magari na pikipiki zimeshuhudiwa katika baadhi ya Vituo vya mafuta Zanzibar baada ya kutokea kwa uhaba wa mafuta ya petroli ambao Mamlaka inayohusika na masuala ya mafuta (ZURA) ilisema upungufu huo umetokana na kuchelewa kwa meli ya mafuta Zanzibar.
“Kulijitokeza upungufu wa mafuta ya Petroli katika baadhi ya Vituo Zanzibar kumesababishwa na kuchelewa kufika kwa Meli ya mafuta kutoka Tanga ilikokwenda kupakia mafuta, Meli hiyo imefanikiwa kufika salama Mtoni Zanzibar usiku wa Jumatatu April 15”
Licha ya taarifa hiyo ya ZURA bado foleni imeshuhudiwa katika baadhi ya Vituo vya mafuta Zanzibar