Waziri wa Madini, Dk Doto Biteko ni mojawapo wa viongozi walioshiriki katika mkutano wa wakuu wa Serikali ya Russia na nchi za Afrika uliaonza Julia 27 hadi 29 maka huu 2023 katika Jiji la St. Petersburg nchini humo.
Biteko aliwaeleza washiriki wa mkutano huo kuhusu fursa zilizopo katika sekta ya madini ili kuvutia uwekezaji ambapo ameyataja baadhi ya maeneo kuwa ni pamoja na shughuli za utafutaji, uchimbaji, uchenjuaji, uongezaji thamani madini na biashara ya madini nchini.
Washiriki wengine katika mkutano huo ni pamoja na wafanyabiashara na watu mashuhuri kutoka Russia na nchi za Afrika.