Menu ›
Biashara
Wed, 25 Oct 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Exaud Kigahe ametoa rai kwa Watanzania kununua bidhaa zinazotengenezwa na viwanda vidogo nchini ili kupanua wigo wa masoko ya bidhaa, kuongeza uzalishaji kukuza viwanda hivyo.
Kigahe ameyasema hayo wakati akifungua Maonesho ya nne (4) ya Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo (SIDO) Kitaifa yanayofanyika katika Viwanja vya Sabasaba Mkoani Njombe.
Pia ameielekeza SIDO kushirikiana na Halmashauri zote nchini kuzalisha kwa wingi teknolojia na zana za kisasa zitakazosaidia katika uzalishaji na usindikaji wa bidhaa.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live