Menu ›
Biashara
Mon, 16 Dec 2019
Chanzo: mwananchi.co.tz
Dar es Salaam. Waziri wa Kilimo, Japhet Hasunga kesho Desemba 16 atazindua Mkakati wa kuendeleza zao la mpunga awamu ya pili 2019-2030, jijini Dodoma Tanzania.
Taarifa iliyotolewa leo Desemba 15 na Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo, Mhandisi Mathew Mtigumwe imesema mkakati huo utatekelezwa kwa kipindi cha miaka kumi kuanzia 2019/2020 hadi 2029/2030.
“Uzinduzi huo utafanyika katika ukumbi wa mikutano wa St Gaspar Jijini Dodoma kuanzia saa 2.00 asubuhi. Wadau wa zao la mpunga na wananchi mnaalikwa,” imesema taarifa hiyo.
Chanzo: mwananchi.co.tz