Biashara

Habari

Burudani

Michezo

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Waziri Biteko akabidhi leseni 11 vikundi 10 vya wachimba dhahabu Nzega

87655 Pic+biteko Waziri Biteko akabidhi leseni 11 vikundi 10 vya wachimba dhahabu Nzega

Thu, 12 Dec 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Nzega. Waziri wa Madini Doto Biteko amesema ataendelea kuzungumza kwa namba (takwimu) badala ya maneno huku akitamba kuwa wizara yake itavuka malengo ya makadirio ya makusanyo ya fedha zilizopangiwa na wizara yake kukusanya ambayo ni Sh475 bilioni katika mwaka wa 2019/20.

Waziri huyo ameeleza kuwa dalili za kufikia lengo hilo zimeshaonekana kufuatia kukusanya Sh205 bilioni kwa kipindi cha miezi mitano.

Biteko aliyasema hayo wilayani Nzega wakati akikabidhi  leseni 11 kwa vikundi 10 vya wachimbaji wadogo wa madini ya dhahabu.

Biteko amesema uthubutu wake na viongozi wenzake wa wizara nzima ndio unaopelekea kuiweka sekta ya madini kwenda mwendo mdundo  huku akiahidi yeyote anayetaka kurudisha nyuma mwendo huo hatokubaliana nae.

 “Madini haya si yangu mimi wala ya Rais John Magufuli, ni madini ya Watanzania na sote tunawajibu wa kuyalinda, kazi yangu ni kusimamia maekezo ninayopewa na rais  ni  kuhakikisha sekta hii inachangia kwenye pato la taifa kama inavyostahili.

“Narudia tena, anae stahili sifa katika haya yote yanayofanyika kwenye madini sio Mimi Doto Biteko, anaye stahili sifa na pongezi zote ni Rais John Pombe Magufuli kwani yeye ndiye anaye elekeza na mimi ni msimamizi tuu wa kutekeleza yale anayo yaagiza.”. amesema Biteko.

Biteko amesema amekuwa akipata simu kadhaa za wananchi wakimpa taarifa za utoroshaji wa madini lakini huwa anachukizwa  na vitendo vya uchonganishi kutokana na baadhi ya watu kutoa taarifa za uongo.

Katika hafla hiyo Biteko alikabidhi leseni kwa vikundi 10 ambavyo ni  Msilale Miners Group, Jimbo la Nzega Vijijini, Undomo Miners Group, Hapa Kwetu Group, Umoja wa Wachimbaji Mwanshina, Mkombozi Mining Group, Imalamakoye Miners Group, Salama Miners, Makalanga Minerals Group na Nzega Miners Association.

Chanzo: mwananchi.co.tz