Biashara

Habari

Burudani

Michezo

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Watalii 10,000 kutoka China wazuiwa kuingia Tanzania

93298 Pic+watalii Watalii 10,000 kutoka China wazuiwa kuingia Tanzania

Tue, 28 Jan 2020 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) imesitisha watalii 10,000  kutoka China kuingia Tanzania kwa ajili ya kudhibiti maambuzi ya virusi vya corona yaliyoikumba nchi hiyo ya bara la Asia.

Watalii hao walikuwa wanaletwa Tanzania na kampuni ya  Touchroad International  Holdings Group.

Taarifa iliyotolewa leo Jumatatu Januari 27, 2020 na mwenyekiti wa bodi hiyo,  Jaji Thomas Mihayo inaeleza kuwa wamesitisha ujio wa watalii hao baada ya Serikali ya China kuzuia wananchi wake kusafiri nje ya nchi hiyo kutokana na mlipuko wa ugonjwa huo.

Jaji Mihayo amesema Desemba 2019 bodi hiyo na kampuni ya Touchroad waliisaini makubaliano ya ushirikiano wa kuleta  watalii 10, 000 kutoka China.

"Napenda kuchukua fursa hii kwa masikitiko kuwajulisha safari hizo za ndege  maalumu za ATCL kuleta watalii zilizopangwa kufanyika Februari 24 na Machi 2, 2020  zimeahirishwa baada ya serikali ya China kuzuia wananchi wake kusafiri nje ya nchi hiyo,” anaeleza Jaji Mihayo katika taarifa hiyo.

Amesema kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa mwenyekiti wa kampuni hiyo, ujio wa watalii hao umezuiwa kudhibiti kuenea kwa virusi hivyo.

Pia Soma

Advertisement

Chanzo: mwananchi.co.tz